Anaandika
@aman_martins
.
2016 nilikwenda Dodoma kuripoti habari za Bunge mara ya kwanza. Kwenye mgahawa mmoja, Prof Jay anakubali kuonana nami na kunipa ananipa stori za maisha yake.
.
Alama yake katika maisha ya Watanzania, iko kwenye Muziki alioanza mwaka 1989, kisha 1994 alipojiunga Hard Blasters Crew, kabla ya kutubariki na album 6 na Nyimbo kibao.
.
Anafahamika sana kwa haya:
.
1. KAHESHIMISHA #HIPHOP:
@adamchomvu aliwahi kusema “Credit kubwa ya Prof ni jinsi alivyowafanya watu wote hata wazee kuona huu sio mziki wa Kihuni”. Kauli hiyo nimeisikia na kuithibitisha kupitia wajuzi wengine pia wengi wakisema ngoma yake ‘Chemsha Bongo’ ni kati ya mifano mizuri ya ngoma zilizopenya kwa rika zote.
.
2. KIPAJI CHA KIPEKEE: Nilimsikia Prof mwenyewe akisema “Hakuna msanii wa Hiphop anayefanya kitu ambacho leo ambacho me sikufanya tangu zamani”. Vitu hivyo ni vya kuhusu muziki tu kwa maana ya flow na maudhui. Wewe fuatilia utagundua hili ni la ukweliz Prof kaimba vitu vingi mnooo, na hadi leo anafanya hivyo.
3. UTU: Prof ana kila sababu ya kupandisha mabega, lakini siku zote anajishusha.Ndio maana katika matatizo yake, watu wengi walikuwa karibu yake, mtu wa watu kwelikweli.
.
Pamoja na yote, andiko hili ni maalum kwa #Wapambanaji wengi wanaopitia Magumu. Labda umeunguka kimaisha, au unaumwa: mtazame
@professorjaytz
.
Katika nyakati ambazo kila mtu alikata tamaa, ukuu wa Mungu ulidhirihirika. Siku 462 hospitali (alikaa ICU siku 127) ziwe tumaini na ukumbusho kwako kwamba huo sio mwisho, usijikatie tamaa, utasimama tena.
.
#Champ, #JaridaLaChamp. 23/09/2025