Baada ya jana team XXL kuzungumzia kipande kilichopo kwenye Filamu ya wasifu(Biopic) ya Michael Jackson ambacho hifadhi ya taifa Serengeti ilitajwa na kusifiwa, Leo Katibu mkuu wa wizara ya maliasili na utalii @dktabbasi kwanza ameishukuru team XXL kwa kuwapa habari hiyo njema lakini pia amesema wameshaanza mazungumzo na Jafar jackson(ambaye aliigiza kama michael jackson) pamoja na producer wa Filamu hiyo kuwakaribisha katika hifadhi ya taifa Serengeti, msikilize akifunguka zaidi leo kwe XXL.
Hyper man @iddy_muller ametoa exclusive ndani ya #DoubleXL kuhusu ku-host tamasha ambalo litaandaliwa Las Vegas Marekani. Ametoa shukrani zake pia kwa @snipermantana kwa kumfungulia Dunia.
Mashabiki wa soka na muziki duniani wameanza countdown rasmi baada ya taarifa kuthibitisha kuwa superstar wa kimataifa Shakira ameungana na staa wa Afrobeats Burna Boy kwenye anthem mpya ya FIFA World Cup 2026 inayojulikana kama “Dai Dai.” #Whatspoppin