It's time to enjoy.....kwa mara nyingine Tena inashushwa burudani muendelezo...
#Bombambaya tour inaendelea kwa Kasi ya ajabu
And this time around....ni zamu ya MSOWERO
Bonge la burudani linaangushwa katika Ukumbi wa Msangeni Pub(jumba la burudani)
Kiingilio ni TSH 5,000/=
Jukwaa litashambuliwa na watangazaji kutoka Mjengoni Planet Fm na kwa Upande wa burudani itasimamiwa na @basley_bway@jaycombat_@sumadomc
Hii si ya kukosa
Ni tar 30/05/2026
Kituo cha pili kimejulikana rasmi wakazi wa Msowero hii si ya kukosa kabisa hapa tunakuletea Sumado Mc,Baslay Bway na kaka mkubwa mwenye wivu wake Jay Combat kwa mtonyo wa shilingi 5000/= tu
Tukutane katika Ukumbi wa Msangeni Pub tar 30/05/2026
#nibombambayatour
#msowero
Wamiliki wa magari ya uchukuzi wa umma wameitisha mgomo kuanzia leo Jumatatu asubuhi wakishinikiza serikali kufuta nyongeza ya bei ya mafuta iliyotangazwa juma lililopita.
Polisi nchini Kenya wametoa taarifa kuwahakikishia usalama wamiliki wa magari ya uchukuzi wa umma ambao watataka kuendelea na shughuli zao.
Bei ya mafuta ya Disel yaliongezeka hadi shilling 242 huku petroli ikiuzwa hadi shilingi 214 za Kenya 🇰🇪.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Balozi Dk. Bashiru Ally Kakurwa, amesema Mradi wa Kukuza Usimamizi Endelevu wa Uvuvi na Ukuzaji Viumbe Maji wa Bahari Tanzania (TASFAM) ni muhimu katika kukuza Sekta ya Uvuvi, kisayansi.
Waziri amebainisha hayo katika mahojiano maalum baada ya kupitishwa kwa Mpango na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa Mwaka 2026/27 ya wizara hiyo, bungeni jijini Dodoma Mei 14, 2026 ya Shilingi Bil. 433, ambapo amesema TASFAM itajikita katika utafiti na mafunzo.
Ameongeza kuwa TASFAM, inalenga kuwawezesha wavuvi na wakulima wa mwani katika Ukanda wa Pwani kutumia teknoloijia za kisasa katika mazao ya uvuvi kikiwemo kilimo cha mwani na walengwa wakubwa ni vijana na akinamama huku ikizingatia uhifadhi wa mazingira na kutoa elimu na mafunzo kwa vitendo.
Mradi wa TASFAM unatekelezwa katika halmashauri za wilaya 16 zilizopo katika mikoa ya Tanga, Dar es Salaam, Pwani, Lindi na Mtwara katika kipindi cha miaka mitano kwa thamani ya Dola za Kimarekani Mil. 117
Katika muendelezo wa soka leo
@Simbasportsclub atakuwa dimbani akimkaribisha @Traunited katika uwanja wa KMC complex
Yote ni kusaka tiketi ya kucheza nusu fainali kombe la #crdbfederetioncup2026
Planet fm tutakuletea matangazo ya Moja kwa Moja
Weka utabiri wako
Mheshimiwa Gerson Msigwa alivyoufikisha Ujumbe wa Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na MichezoUJUMBE MHE.PAUL MAKONDA Kwenda kwa Mheshimiwa Tulia Akson na wana Mbeya.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Mfanyabiashara kutoka nchini Nigeria ambaye pia ni Mwanzilishi na Mmiliki wa Dangote Group, Alhaji Aliko Dangote pamoja na Ujumbe wake, Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 16 Mei, 2026
Habari picha:
Mbunge wa Uyole na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani ( IPU ) Mheshimiwa Tulia Akson katika na Mgeni Rasmi Mheshimiwa Gerson Msigwa katika msimu wa kumi wa Betika Mbeya Marathon.
LUGHA YA KISWAHILI KUFUNDISHWA NCHINI URUSI Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) Bi. Consolata Mushi pamoja na Waziri wa Maendeleo ya Uchumi wa Shirikisho la Urusi Bw.Maxim Rshetniokov wakisaini Mkataba kuhusu Lugha ya Kiswahili kuwa miongoni mwa lugha itakayofundishwa nchini Urusi.
Tukio hilo limefanyika tarehe 16 Mei, 2026 katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Jijini Arusha wakati Kikao cha Tatu cha Tume ya pamoja ya Kimataifa ya Ushirikiano wa Biashara na Uchumi kati ya Tanzania na Urusi ambacho kimekutanisha Viongozi wa Serikali, Wafanyabiashara na wadau mbalimbali.
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Paul Makonda ameshuhudia tukio hilo.