Tuliufahamu upande mmoja wa maisha yake ya Muziki wa Bongo Fleva alipokuwa Tanzania, Jumapili hii @vanessamdee yuko tayari kufunguka kuhusu maisha yake mapya ya wokovu, huduma, malezi na familia kwa ujumla.
Usikose kusikiliza #GospelTraxx ya CloudsFm kuanzia saa 12:00 asubuhi na tutakuwa LIVE pia kupitia YouTube ya CloudsMedia
Cc: @hurumacharles@favvie_tz@djsamgram@yuda_jay@pastordolaa@cloudstv
Fedha ina nafasi gani katika ndoa? Je ndoa inaweza
kuharibika kwa sababu ya fedha?
Tukutane kesho kwenye #GospelTraxx ya Clouds Fm na Mwanasaikolojia @chrismauki_ kuanzia saa 12 asubuhi na
tutazungumzia fedha na Mahusiano.
Unaweza pia kufutilia Live kupitia YouTube ya CloudsMedia
Cc: @hurumacharles@favvie_tz@pastordolaa@yuda_jay@djsamgram
Mhubiri Pastor Iman Mwakanyamale @iman_mwakanyamale kutoka Building The Temple of God (BTG) Ministry @btg.ministry amesema Yesu atakuja wakati wa amani na sio kama watu wanavyofikiri sasa kuwa atakuja wakati wa matukio.
#GospelTraxx
"Mitandao naitumia kwa ajili ya kazi na kazi yangu ni Injili. Kuna watu hawajui kama nina mtoto lakini nina mtoto na hii ni kwa sababu unapo-expose baadhi ya vitu unaruhusu vita ambayo wengine hawako tayari kupigana nayo. Mfano mimi nikiposti picha yangu ukanitukana nimejiandaa kwa hilo lakini mke wangu au mtoto wangu utakuwa unawatesa kisaikolojia kwa sababu hawajajiandaa na hiyo vita. Wakiwa wamejiandaa vya kutosha na wako tayari kupigana hiyo vita naweza kuwaposti.
Sio kila vita lazima upigane. Kuna vita nyingine zinakuja kwa ajili ya kukutoa kwenye mstari sio lazima upigane. Vita nyingi ambazo tunapigana zimeletwa kwa ajili ya kutupotezea muda" - Mhubiri Pastor Iman Mwakanyamale @iman_mwakanyamale kutoka Building The Temple of God (BTG) Ministry @btg.ministry
#GospelTraxx
Karibu kwenye #GospelTraxx ya Koinonia yaani #GospelTraxx ya ushirika na Roho Mtakatifu na yapo mengi kwa ajili yako Jumapili hii kuanzia saa 12:00 asubuhi mpaka saa 3:00 asubuhi.
#GospelTraxx
Shalom Choir kutoka Kibamba Assemblies of God (TAG), watakuwa nasi kwa ibada ya kumsifu Mungu! f
Jiandae kwa muziki mzuri wa injili na mambo mengi mazuri. Ni kuanzia Saa 6:00 asubuhi mpaka 9:00 asubuhi!
Cc @tagkibamba321@hurumacharles@favvie_tz@yuda_jay@djsamgram@justdolaa
Beda Andrew, @bedaandrew Mwimbaji wa Injili mwenye sauti ya kipekee na ujumbe wa kumgusa kila mmoja.
Jumapili hii Beda Andrew atakuwa na jambo lake mwenyewe siku ya
Leo pale Makumbusho ya Taifa Posta akiwa na theme isemayo “Right
Moment / Wakati Sahihi”, akiwa na Watumishi mbali mbali.
Mengi utayajua Zaidi Kwa Jiunge nasi hapa Clouds Fm tukimsifu
Mungu kupitia nyimbo za kuinua mioyo na mahojiano ya kina kuhusu huduma yake. Usikose kuungana nasi Clouds FM radio pia cloudsmedia YouTube kuanzia saa 6:00 hadi 9:00 asubuhi!
Cc @yuda_jay@pastordolaa@djsamgram@favvie_tz@hurumacharles
Jumapili hii kwenye Gospeltraxx, Mhubiri Pastor Iman Mwakanyamale kutoka Building The Temple of God (BTG) Ministry!
Atashirikisha nasi ujumbe muhimu kuhusu End-Time Awakening (Uamsho wa Siku za Mwisho). Ujumbe huu ni wa kipekee na unalenga kutuandaa kwa nyakati za mwisho. Umejiandaaje??
Ungana nasi Clouds FM radio ya watu au cloudsmedia YouTube, kuanzia saa 6:00 hadi 9:00 asubuhi!
[email protected] na @iman_mwakanyamale kwa mafundisho zaidi.
#GospelTraxxCloudsFm
Kama ulikuwa unawaza kama matamasha ya Injili yanaingia faida basi tumemuuliza Mkurugenzi Yona Sonelo (Rungwe} walitumia gharama kiasi gani kumleta Mercy Chwino?
Ametujibu: "Kumleta Mercy Chwino ilitumika Milioni 190, na katika viingilio ilipatikana milioni 80. Na tulimleta Mercy kwa sababu tulifanya uchunguzi na kuuliza watu ambao wamezama sana katika Gospel nani anapendwa kwa sasa kwa sababu hadi wanaopenda mziki wa dunia wanasikiliza mziki wa Injili kwa sasa"
#GospelTraxx