Mama na Mwana Bungeni Dodoma
Mbunge wa Mchinga Mama Salma Kikwete ambaye ni mke wa Rais Mstaafu Kikwete(katikati), kushoto ni mtoto wake Ridhiwani Kikwete Mbunge wa Chalinze, na Mbunge wa Shinyanga Mjini, Patrobas Katambi katika viwanja vya Bunge Mapema leo.
Cc @ridhiwani_kikwete@salma_kikwete@patrobasskatambi_
Kila jambo na wakati wake, hii ni kubwa sana kwangu kutoka kwa @diamondplatnumz .
Asante kwa kunipa nafasi mara zote, usichoke kutoa support kwa vijana wapambanaji ambao tunatamani nafasi zaidi za kukua.
Nitaendelea kuamini na kusimama kwenye uandishi wa habari unaohudumia Umma kwa Heshima, Uadilifu na Usawa.
🙏🏿🙏🏿🙏🏿🙏🏿 @diamondplatnumz
🎥 by @wcb_wasafi@wasafigallery
Ajali iliyoua watatu Dodoma, kijana aiba rimu ya gari ambalo dereva amefariki na makonda wake wawili, Wananchi waanza kumkimbiza.
Hata mimi nilikuwa sijui tunakimbiza nini 😂😂, mbele ya safari nikaambiwa tunamkimbiza mwizi dah.
Niliamua kutoa vyeti vya heshima kwa wasanii waliofanya mambo makubwa kwenye tasnia ya Sanaa, wengi walinipa nafasi katika safari zao, sasa licha ya kuwa mastaa ila pia ni source wangu muhimu sana.
Nikaona nifanye nao interview special ‘BongoKings’ na kuwapa vyeti vya heshima, ingawa project ‘’ imeishia katikati.
Mmoja ambaye nilimfikia ni @zahirzorro , ni mwamba sana kwenye hii tasnia ya muziki.
Licha ya changamoto ya kiafya ila ulinipa nafasi ya kufanya mahojianao na wewe, ni heshima kubwa sana wala siichukulii poa.
Mungu akupe afya njema, kazi uliyoifanya haiwezi kufutika.
Mnawaonea sana watoto 2000, umekutana na wamjini 20 una generalized wote.
Kwa mujibu wa studies, wanasifa nyingi ila nimekuwekea hizi
1. Wanatafuta usalama wa kiuchumi na hapendi kuingia kwenye hatari za kimali.
2 Ni wabunifu , wanapenda kujifunza vitu mwenyewe, na wana malengo makubwa ya kazi.
3. Wanakubali utofauti wa watu na hapendi ubaguzi au mifumo ya kizamani.
4. Wanajali sana ustawi wao wa kisaikolojia na anajua umuhimu wa kujitunza.
Una mtazamo gani?
Wiki hii nikiwa mzigoni Bungeni Dodoma, nimekutana na Senior Lecture wa SJMC, Dr. Dotto Paul Kuhenga. Kukutana naye kumenikumbusha mambo mawili makubwa kuhusu Media Criticism moja ya somo ambalo alinifundisha, na nikafikiria haya.
Political Economy of the Media (Uchumi wa Kisiasa wa Vyombo vya Habari) in Agenda Setting na Framing.
Umiliki wa chombo cha habari na maslahi ya kifedha (matangazo au siasa) ndivyo vinavyoamua habari gani ichapishwe.
Nikaangalia waandishi waliokuzunguka hapo Bungeni. Wale wa vyombo binafsi wanatafuta habari gani? (Zenye drama ili wapate ‘clicks’ na watazamaji wengi).
Wale wa vyombo vya serikali wanaripoti vipi? (Wanasisitiza mafanikio).
Media criticism inakusaidia kuona jinsi fedha na nguvu ya kisiasa inavyoendesha kalamu za waandishi.
Asante sana Dr. Dotto
Kama huwezi kuwashinda, basi ungana nao
Trump kusafiri na CEOs wakubwa ni sehemu ya diplomasia ya biashara na uchumi. Safari hizi mara nyingi huwa na malengo kadhaa: • Kufungua biashara mpya kati ya nchi mbili • Kujadili uwekezaji mkubwa • Kushawishi sera za biashara au ushuru (tariffs) • Kulinda maslahi ya kampuni za Marekani nje ya nchi • Kuonyesha nguvu ya kiuchumi ya Marekani
Katika safari yake ya hivi karibuni kwenda China, Trump aliambatana na CEOs wa kampuni kubwa kama Elon Musk, Tim Cook, na Jensen Huang. Ripoti zinaonyesha walikuwa wanajadili masuala ya: • biashara kati ya Marekani na China, • AI na teknolojia, • viwanda na supply chains, • pamoja na uwekezaji mpya.
Kwa upande mwingine, watu wengine wanaona hii kama: • Trump kutumia urafiki wake na wafanyabiashara wakubwa kuongeza ushawishi wake, • au kuifanya safari ya kisiasa ionekane kama “mission ya biashara.”
Kwa kifupi:
Trump husafiri na CEOs kwa sababu viongozi wa biashara wana nguvu kubwa kwenye uchumi, ajira, teknolojia, na uwekezaji.
Hivyo safari za kimataifa mara nyingi huwa si za siasa tu bali pia biashara.
Nikasema nifuatie kidogo mkutano huu wa wakubwa wawili duniani