Ubao unasema dakika ya 89 Yanga walikua wanaongoza 1-2 lakini Full Time ubao ulisomeka 3-2 madogo wameshinda
Hii picha ukija kuwaonyesha wajukuu zako na kuwaambia Yanga alikufa 3 unaweza kubishana nao mpaka uwaletee ushahidi..
Tuachane na hayo
Mwenye namba ya kapteni Beka anipe nataka nimtumie chochote kitu kafanya la maana sana kwetu 😂
Mwenye namba ya Waziri Jr pia anipe nae anastahili kutumiwa ya soda kazima kelele mjini kafanya la maana sana 😂
Aliye karibu na Diarra amwambie wanaume hawasusi ona sasa kawatoa wenzie mchezoni 😂
SIMBA KAMA TRENI LA UMEME
Na #Abdul_Jembe
Naam Simba na kasi ya train la umeme ukingoni mwa msimu
Kassali kabla na baada ya kucheza vyema mchomo wa Mgunda alikua amepumzika tu akipasiana mali na mabeki wake
Waziri wa ulinzi Ismael Olivier Toure anaihakikishia Simba usalama hata wakati huu ambao Rushine hayupo dimbani,madogo kina Masinde, Duchu, Kibabage pamoja na Mligo wanakua chini ya uongozi wake akiwatuliza na kuwapanga ili kuiweka timu salama..
Mwamba ana uwezo wa kucheza mipira juu,ya chini, kukabiliana, kuingia uvunguni, kupandisha timu na kupiga pasi kwa usahihi, usajili wake ulikua muhimu sana tumemsahau Nangu na sasa hayupo Rushine bado tupo salama ahsante Barker kwa kutuletea huyu mwamba..
Dimbani yupo Kagoma anakata umeme afu maestro Maema the passer anasambaza tu upendo kwa pasi zake..
Lile assist la maestro Maema kwa Mwalimu ni bonge la pass 🔥🙌, bila ajizi nae Mwalimu anamalizia vyema.. What a finish 🔥🙌
Hii Simba ya asali na maziwa ni kama Cruise Ship (Meli kubwa kabisa) inayofukuzia Mtumbwi (Yanga) katika mawimbi makubwa deep see nini kitatokea? 😂 usinipe jibu..
Full Time
Mashujaa 0-3 Simba
Remember the name
Clatous Chota Chama (Magician)
Ukipenda unaweza kumwita Mr Simba
Alichokifanya sina sababu ya kusema sote tumejionea, leo amechukua tuzo yake ya nne mfululizo ya MOTM kuanzia game dhidi ya Yanga, JKT, Prison na hii Mashujaa bila shaka ni mchezaji bora wa mwezi..
Nina mengi ya kusema lakini ngoja niishie hapa
Niite #Baba_Ammar
Kipa bora wa ligi kuu ya Uingereza (EPL) kwa mara ya tatu mfululizo.. What a records 🔥🙌
Raya msimu huu EPL ana clean sheets 18 ikiwa zimebaki mechi mbili inawezekana akafikisha 19 au 20
Hizo clean sheets 18 ni sawa na ushindi wa Man Utd mpaka sasa wameshinda mara 18 😂
Sitashangaa mwisho wa msimu nikiona Raya ana clean sheets nyingi zaidi ya ushindi wao 😂
Ukiwa na kipa kama hili afu linalindwa na watu kama Big Gabby, Saliba, Timber, Calafiori,Hincapie ,Ben, White, Mosquera bila kumsahau kamanda wa vita Rice unategemea nini?
Wanastahili haya mataji..
Three Important Points With Clean Sheet As Usual
Na #Abdul_Jembe
Naam ni alama 3 muhimu bila kuruhusu goli kama kawaida
Kamanda Raya katika milingoti mitatu akiwa na wanajeshi wake Ben White, Mosquera, Calafiori, Skelly, Saliba na Big Gabby wakisaidiwa vyema na kamanda Rice kutoka katika eneo la kiungo..
Mechi ilianza kwa kasi sana Arsenal wakihitaji kupata magoli ya mapema, Calafiori alijaribu kupiga mashuti mara kadhaa lakini haikuwa bahati yake pia Trossard alijaribu mara mbili kichwa chake cha kwanza kikiokolewa na kipa na cha pili kikigonga mwamba..
Baada ya kuumia White sikuona sababu ya kuingia Zubimendi na Rice kutoka kwenye eneo la kiungo na kwenda kucheza beki mbili hayakuwa maamuzi mazuri yalidhoofisha eneo la kiungo mpaka ikapelekea baadae kumtoa tena Zubimendi na kuingia Ode pamoja na Kai
Kutokana na sub ile ya kujichanganya ya White kwa Zubi mpaka wakajikuta wanalazimika kumtoa Calafiori aingie Mosquera na ikapelekea Skelly kujikuta anarudishwa kucheza beki 3 eneo ambalo kwa sasa ni Calafiori na Hincapie peke yao wanacheza..
Alipoumia White moja kwa moja alitakiwa kuingia Mosquera sio lazima Zubi acheze Arteta na jopo lake walifanya makosa..
Subs za Odegaard na Kai zilisaidia timu na walikuja kufanya vyema hasa Ode alikuja na funguo ya kufungulia ushindi hata assist ilitoka kwake kwenda kwa mfungaji Trossard ambaye alikandamiza mpira ambao uliwashinda beki ambaye ali-slide kuzuia pamoja na kipa golini
Raya na mabeki wake 🔥🙌
Gabriel namtaja tena peke yake japo yupo katika jopo la Raya 🔥🙌
Trossard 🔥🙌
Rice 🔥🙌
Odegaard 🔥🙌
Kazi imeisha acha haters walie lie inafurahisha
Naweka kalamu chini
#COYG 🔴 ⚪ 💪
Niite #Baba_Ammar
Mwamba alikiwasha sana Euro 2000 pale France na France kuwa mabingwa wakiichapa Italy katika final na yeye ndio alifunga goli la kusawazisha dakika za baada ya Italy kuongoza kwa muda mrefu na goli lake ndio lilirudisha matumaini na kuwafanya France wapate goli la ushindi kupitia David Trezeguet ambaye alipokea pasi (assist) kutoka kwa Robert Pires
Mwamba amefanya mengi Arsenal lakini kitu cha ambacho tunakikumbuka zaidi ni pale alipotufungia goli pakee la ushindi pale OT 2002 na tukatangazia ubingwa pale na kupiga parade la maumivu uwanjani kwao
Call him Sylvain Wiltord
Miss you nigga
Happy birthday legend
Alijiunga na Arsenal mwaka 1995 msimu mmoja nyuma kabla ya Wenger kutua 1996 na hakuhama mpaka alipostaafu baada ya final ya Uefa Champions League 2006
Mchezaji wangu bora zaidi Arsenal na ndio number 10 wangu bora muda wote EPL mzee wa magoli ya kukuacha mdomo wazi na assists za maajabu zinawezoweza kukufanya utikise kichwa
Ni mmoja kati ya wachezaji watatu ambao wamejengewa masanamu pale Emirates Stadium
Ni mmoja kati ya wachezaji wachache wanaoburudisha wakicheza, wakifunga na kutengeneza magoli..
Mwite Dennis Bergkamp the flying Dutchman 🔥
We miss you our legend
Happy birthday Maestro Bergkamp
Long life Magician
List ile ile ambayo iliwanyonga Fulham kisha ATM na sasa inaenda kutupa matokeo mengine mazuri In Shaa Allah
Raya na walinzi wake wanne Ben White, Calafiori, Saliba na Big Gabby wataendelea kulinda amani yetu..
Katika midfield mwamba Rice yupo na mafundi left footer Skelly na maestro Eze..
Kule juu three attacking soldiers kulia Saka kushoto Trossard kati bulldozer Gyokeres
Angalia benchi lilivyokua na watu wazito 💪
Kila la kheri wapambanaji wetu
#ComeOnYouGunners 🔴 ⚪ 💪
Tangu Upton Park mpaka sasa London Stadium Arsenal siku wakitoa macho matokeo huwa ni mabaya sana kwa West Ham
Ni ukweli usiopingika hii mechi huwa ni ngumu sana ni London Derby hii lakini siku zote mkubwa mkubwa tu ndio maana hapo chini unaona dozi za 2-5 na 0-6 pale pale barazani kwao
Hiyo mechi ya 0-6 mpaka Half Time Arsenal alikua anaongoza 0-4 mashabiki wa Hummers wakaondoka wengi sana uwanjani katika kipindi cha kwanza baada ya maumivu ya kipigo kikubwa ndani ya First Half
Leo ni mechi yenye hisia zaidi sababu kila timu ina lengo lake kubwa sana na muhimu sana katika msimu wakati West Ham wanataka kujinasua katika janga la kushuka daraja Arsenal wao wanataka ubingwa muhimu sana baada ya miaka lukuki bonge la mechi
Leo Spurs wapo njia panda sana ukisikia ukisimama nchale, ukikaa nchale na ukikimbia nchale ndio hii sasa, ushindi wa Arsenal ni nafuu kwao katika kubaki Epl lakini pia ni maumivu makubwa Arsenal kuwa mabingwa watajua wenyewe waombe dua gani..
Kila la kheri Arsenal
#ComeOnYouGunners 🔴 ⚪ 💪
Hawa viande Chelsea leo wamenusurika na kipigo kama walivyozoea
Midomo Fc leo wamesagana kipa wao kapata sana shida na nyingine zimekula nguzo matokeo haya buyu buyu ni bahati kwao
Wengi katika kuuficha ubora wa Arsenal wanapost na kuzungumzia matokeo ya mechi mbili tu ambazo PSG walishinda ila haya matokeo hawayaongelei kabisa kama sio ya msimu jana
Hii ndio mechi Arsenal walikuwa full mkoko Gabriel Magalhaes ndani PSG alichezea kamba 2-0 na lile jini Donnarumma lilitoa michomo mingi sana ya kina Marinelli otherwise zilikua nyingi
Mechi mbili za semi-finals Arsenal walikua na majeruhi wengi na nafasi ya Gabriel alicheza Jakub Kiwior lakini bado hizo mechi zote zilikua ngumu sana kuanzia Emirates mpaka kwao na Donnarumma aliendelea kuwa shujaa wao jiulize wangekua full mziki na Gaby ndani ingekuwaje pengine Aggregate ingekua 1-1 au tungeshinda kabisa
Siwezi kusahau lile kamba la bichwa la kikatili ambalo aliwaua Merino akiwa amezidi vidole tu tunanyimwa goli tamu sana pale Emirates
Nakupa Aggregate ya jumla mechi zote 3
England
Arsenal 2-0 PSG
Arsenal 0-1 PSG
France
PSG 2-1 Arsenal
Aggregate
Arsenal 3-3 PSG
Bahati kwao PSG matokeo mazuri waliyapata katika mechi za mtoano, lakini watu washajisahaulisha ilikuwaje wanatufananisha na Inter, Chelsea na viande wengine eti oooh mtapigwa 5-0 sijui 7-1 wengine 8 nawaangalia tu,lini mmesikia hii Arsenal shindani ikipigwa hata 4? hata yale magoli manne ambayo PSG waliyaruhusu kwa Bayern wakiwa kwao sisi kwetu hilo haliwezekani waulize Bayern hata hilo 1 hawakuamini walipopata tulipowachapa 3-1..
Wakifanya makosa ya kuruhusu kijinga wasitegemee kufunga mengi imekula kwao sisi sio kama wengine
Mliyo na matokeo yenu katika nyoyo zenu chungeni msije kuzimia/kufa kwa presha tukichapa huyu mnayemtegemea kulinda furaha zenu na amani yenu ya moyo
Waleteni wakali wenu
Waleteni wababe wenu
Mwanzo tuliambiwa hata kama tumeingia final lakini hatuwezi kukabiliana na yeyote kati ya Bayern au PSG
Lakini ukifuatilia kwa kina maneno yao (UKAWA) baada ya PSG kufanikiwa kuingia final unagundua hata huyo Bayern walikua hawamuamini dhidi ya hii Arsenal yenye maajabu
Angalia balaa lilofanyika katika hizo mechi 14 sio mchezo linaogopesha so wanaponda huku wanatetemeka na kuogopa, katika hizo mechi 14 Bayern pia yupo humo alichezea 3-1 nawaelewa mnavyohofia..
Tunamuheshimu sana PSG na tunajua haitakua rahisi na hatutegemei kuwa mabingwa kirahisi so tumejiandaa kupambana kwa ajili ya ushindi
PSG sio maroboti wala sio majini na hawana miguu minne minne ni timu yenye ubora ambayo inafungika ikiwa una timu bora na mikakati nasi tuna vigezo hivyo,timu tunayo, nia tunayo, mashabiki wa hamasa tunao na sababu pia tunayo na huu ndio wakati wetu..
Nyie malizeni tu maneno sisi kama tulivyoanza tuliwajibu kwa vitendo kila mechi ambayo mlitubeza mpaka tunaingia final hatujapoteza hata mechi moja mnabadilisha tu maneno, sababu na timu za kushangilia sasa matumaini yenu yote yapo kwa PSG na hii pia tutawajibu kwa vitendo
Haya ni mapokezi ya wachezaji pamoja na benchi la ufundi la Arsenal kutoka kwa mashabiki
Ilikua wanawaonyesha wachezaji jinsi wanavyoitaka mechi na wanavyoitaka final
Mapokezi hayo yamefanikiwa kulipa sasa mashabiki, wachezaji pamoja na benchi la ufundi wote wanasherehekea kuingia final
Wakati Arsenal wanashangilia kuingia final ya UCL upande mwingine Man Utd wanashangilia kufuzu tu mashindano hayo tena kwa sherehe kubwa 😂 😂 😂..
Maisha kweli hayana usawa yapo level tofauti baina ya huyu na yule
Wakati huo huo Chelsea yupo nafasi ya 9 huko EPL hajui hata hatma yake itakuwaje maskini..
Hawa hawafai hata kuchekwa tuwaonee huruma tu
Watatii FINALE
Watatupenda FINALE
Referee puliza kipenga FINALE
Round hii tupo FINALE
Tutapambanaa tusipoteze FINALE